Friday, October 14, 2016

KISUKARI ( DIABETES MELLITUS )

Kisukari ni miongoni mwa matatizo ya kiafya yanayowapata watu wengi .Tatizo hili linatokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha sukari kwenye damu (Blood sugar) kuliko mahitaji ya mwili kwa wakati huo kutokana na kushindwa kwa mfumo wa urekebishaji kiwango cha sukari kwenye damu. Baadhi ya viungo vinavyohusika na urekebishaji sukari ni kama vile Kongosho (pancrease) na ini. Kuongezeka kwa sukari kwenye damu kunaweza sababishwa na aidha kongosho kushindwa kuzalisha homoni ya insulin inayosaidia kushusha kiwango cha sukari  (Type I Diabetes mellitus) au Tishu ya mwili kushindwa kuchukua insulinin ili kushusha sukari (Type II Diabetes mellitus).


                  AINA ZA KISUKARI

Kongosho
1.TYPE I DIABETES MELLITUS
  Aina hii ya kisukari hutokana na kongosho kushindwa kuzalisha hormone ya insulin kutokana na kuharibiwa kwa beta cells zinazozalisha hormone hii na kufanya mwili kushindwa kushusha kiwango cha sukari kwenye damu.


2.TYPE II DIABETES MELLITUS 
Aina hii ya kisukari  hutokea kutokana kushindwa kwa tishu za mwili kuchukua hormone ya insulin ili kushusha kiwango cha sukari (Tissue resistance). Hali hupelekea kongosho kuzalisha insulin kuliko uwezo wake ambapo mwishoni kongosho hushindwa kuzalisha insulin kabisa..
       Kuna sababu  mbalimbali zinazosababisha tatizo la kisukari kama inavyooneshwa hapa chini

SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA KUPATA KISUKARI

                              1.Kuwa na uzito mkubwa kupita kiasi














   2.Sababu za  urithi. Tafiti zinaonesha kuwepo kwa genes ambazo hupelekea kongosho kushindwa kuzalisha insulin kwa watu wenye kisukari ambapo huweza kurithiwa kutoka kizazi kimoja kwenda kizazi kingine.

                   3.Magonjwa ya kongosho kama Pancreatitis

                                                        4.Kutumia kilevi.






                         DALILI ZA KISUKARI



  1. Kuhisi kiu ya maji mara kwa mara
  2. Kunywa maji mengi
  3. Kukojoa mkojo wenye sukari
  4. Kusikia njaa mara kwa mara
  5. Macho kushindwa kuona 
  6. Vidonda visivyopona haraka
  7. Kuwa na uchovu 







        NJIA ZA KUEPUKANA NA KISUKARI



 


  1.  Hakikisha uzito wa mwili wako hauwi mkubwa kwa kufanya mazoezi
  2. Epuka kula chakula kinachoongeza mafuta kupita kiasi
  3. Jenga mazoea ya kupunguza matumizi ya kilevi
  4. Nenda hospitali mara kwa mara kujua hali ya afya yako.



LINKS:
http://www.webmd.com/diabetes/guide/types-of-diabetes-mellitus

https://www.betterhealth.vic.gov.au/health/tentips/10-tips-to-help-prevent-type-2-diabetes

Preapared by Andrew Luhusa ,MD Student @MUHAS
              
                               14TH OCT 2016.

Thursday, October 6, 2016

VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCER DISEASE)



Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea kwenye mfumo wa chakula ambapo kuta za tumbo au utumbo hushambuliwa na bacteria waitwao
  helicobacter pylori na kusababisha kuwepo kwa vidonda kwenye kuta za tumbo au utumbo na kuambatana na maumivu makali. Bacteria hawa huweza kukaa kwa muda mrefu ndani ya tumbo bila kuleta madhara hadi pale pindi watakapochochewa kuanza kushambulia kutokana na sababu mbalimbali za kimazingira ,kama utumiaji wa pombe na madawa kama aspirin kwa muda mrefu.
Helicobacter pylori
















SABABU HATARISHI ZINAZOWEZA KUPELEKEA KUPATA VIDONDA VYA TUMBO

1.Matumizi ya dawa aina ya aspirin (Non steroidal anti inflammatory drugs{NSAIDs}) kwa muda mrefu hupelekea kusababisha tatizo la vidonda vya tumbo. Dawa hizi huzuia kutengenezwa kwa kemikali iitwayo prostaglandin ambayo husaidia katika kuimarisha kuta za utumbo . Hivyo kushinndwa kuimarika kwa kuta za tumbo hufanya kuwepo urahisi wa kushambuiliwa na bacteria na kusababisha vidonda.






2.Matumizi ya pombe kupita kiasi husababisha kupungua kwa uwezo wa ndani wa kuta za tumbo (Epithelial lining) kuzuia tindikali ya tumbon kutokuharibu ukuta wa ndani wa tumbo( Mucosal barrier).Hali hii hufanya tindikali pamoja na bacteria kupenya kwa urahisi kuingia kwenye kuta za tumbo na kusababisha vidonda.


stress


3. Uvutaji sigara pia waeza kupelekea kupata tatizo la vidonda vya tumbo.

4.Msongo wa mawazo



DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO

1.Maumivu ya tumbo

2. Kiungulia

3.Kupungua uzito

4.Kichefuchefu na kutapika

5.Tumbo kujaa gas

NAMNA YA KUEPUKANA NA VIDONDA VYA TUMBO

1.Epuka matumizi ya kilevi kupita kiasi


2.Epuka matumizi ya sigara

3.Tumia dawa pale unaposhauriwa na daktari.na epuka matumizi ya aspirin (NSAIDs)

4.Kula chakula bora na mlo kamili usiokuwa na tindikali nyingi.

5.Punguza msongo wa mawazo





LINKS;

1.http://www.webmd.com/digestive-disorders/tc/peptic-ulcer-disease-what-increases-your-risk

2.http://www.healthline.com/health/stomachulcer

3.http://www.mayoclinic.org/diseases-conditions/peptic-ulcer/manage/ptc-20231410

Prepared by Andrew Luhusa; MD student @ MUHAS
                            
                                     7th Oct 2016