
AINA ZA KISUKARI
![]() |
Kongosho |
Aina hii ya kisukari hutokana na kongosho kushindwa kuzalisha hormone ya insulin kutokana na kuharibiwa kwa beta cells zinazozalisha hormone hii na kufanya mwili kushindwa kushusha kiwango cha sukari kwenye damu.
2.TYPE II DIABETES MELLITUS
Aina hii ya kisukari hutokea kutokana kushindwa kwa tishu za mwili kuchukua hormone ya insulin ili kushusha kiwango cha sukari (Tissue resistance). Hali hupelekea kongosho kuzalisha insulin kuliko uwezo wake ambapo mwishoni kongosho hushindwa kuzalisha insulin kabisa..
Kuna sababu mbalimbali zinazosababisha tatizo la kisukari kama inavyooneshwa hapa chini
SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA KUPATA KISUKARI
1.Kuwa na uzito mkubwa kupita kiasi

2.Sababu za urithi. Tafiti zinaonesha kuwepo kwa genes ambazo hupelekea kongosho kushindwa kuzalisha insulin kwa watu wenye kisukari ambapo huweza kurithiwa kutoka kizazi kimoja kwenda kizazi kingine.
3.Magonjwa ya kongosho kama Pancreatitis
4.Kutumia kilevi.
DALILI ZA KISUKARI
- Kuhisi kiu ya maji mara kwa mara
- Kunywa maji mengi
- Kukojoa mkojo wenye sukari
- Kusikia njaa mara kwa mara
- Macho kushindwa kuona
- Vidonda visivyopona haraka
- Kuwa na uchovu
NJIA ZA KUEPUKANA NA KISUKARI


- Hakikisha uzito wa mwili wako hauwi mkubwa kwa kufanya mazoezi
- Epuka kula chakula kinachoongeza mafuta kupita kiasi
- Jenga mazoea ya kupunguza matumizi ya kilevi
- Nenda hospitali mara kwa mara kujua hali ya afya yako.
LINKS:
http://www.webmd.com/diabetes/guide/types-of-diabetes-mellitus
https://www.betterhealth.vic.gov.au/health/tentips/10-tips-to-help-prevent-type-2-diabetes
Preapared by Andrew Luhusa ,MD Student @MUHAS
14TH OCT 2016.