Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea kwenye mfumo wa chakula ambapo kuta za tumbo au utumbo hushambuliwa na bacteria waitwao

![]() |
Helicobacter pylori |
SABABU HATARISHI ZINAZOWEZA KUPELEKEA KUPATA VIDONDA VYA TUMBO

1.Matumizi ya dawa aina ya aspirin (Non steroidal anti inflammatory drugs{NSAIDs}) kwa muda mrefu hupelekea kusababisha tatizo la vidonda vya tumbo. Dawa hizi huzuia kutengenezwa kwa kemikali iitwayo prostaglandin ambayo husaidia katika kuimarisha kuta za utumbo . Hivyo kushinndwa kuimarika kwa kuta za tumbo hufanya kuwepo urahisi wa kushambuiliwa na bacteria na kusababisha vidonda.
2.Matumizi ya pombe kupita kiasi husababisha kupungua kwa uwezo wa ndani wa kuta za tumbo (Epithelial lining) kuzuia tindikali ya tumbon kutokuharibu ukuta wa ndani wa tumbo( Mucosal barrier).Hali hii hufanya tindikali pamoja na bacteria kupenya kwa urahisi kuingia kwenye kuta za tumbo na kusababisha vidonda.
![]() |
stress |
3. Uvutaji sigara pia waeza kupelekea kupata tatizo la vidonda vya tumbo.
4.Msongo wa mawazo
DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO
1.Maumivu ya tumbo
2. Kiungulia
3.Kupungua uzito
4.Kichefuchefu na kutapika
5.Tumbo kujaa gas
NAMNA YA KUEPUKANA NA VIDONDA VYA TUMBO


2.Epuka matumizi ya sigara
3.Tumia dawa pale unaposhauriwa na daktari.na epuka matumizi ya aspirin (NSAIDs)
4.Kula chakula bora na mlo kamili usiokuwa na tindikali nyingi.
5.Punguza msongo wa mawazo
LINKS;
1.http://www.webmd.com/digestive-disorders/tc/peptic-ulcer-disease-what-increases-your-risk
2.http://www.healthline.com/health/stomachulcer
3.http://www.mayoclinic.org/diseases-conditions/peptic-ulcer/manage/ptc-20231410
Prepared by Andrew Luhusa; MD student @ MUHAS
7th Oct 2016
No comments:
Post a Comment