Thursday, October 6, 2016

VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCER DISEASE)



Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea kwenye mfumo wa chakula ambapo kuta za tumbo au utumbo hushambuliwa na bacteria waitwao
  helicobacter pylori na kusababisha kuwepo kwa vidonda kwenye kuta za tumbo au utumbo na kuambatana na maumivu makali. Bacteria hawa huweza kukaa kwa muda mrefu ndani ya tumbo bila kuleta madhara hadi pale pindi watakapochochewa kuanza kushambulia kutokana na sababu mbalimbali za kimazingira ,kama utumiaji wa pombe na madawa kama aspirin kwa muda mrefu.
Helicobacter pylori
















SABABU HATARISHI ZINAZOWEZA KUPELEKEA KUPATA VIDONDA VYA TUMBO

1.Matumizi ya dawa aina ya aspirin (Non steroidal anti inflammatory drugs{NSAIDs}) kwa muda mrefu hupelekea kusababisha tatizo la vidonda vya tumbo. Dawa hizi huzuia kutengenezwa kwa kemikali iitwayo prostaglandin ambayo husaidia katika kuimarisha kuta za utumbo . Hivyo kushinndwa kuimarika kwa kuta za tumbo hufanya kuwepo urahisi wa kushambuiliwa na bacteria na kusababisha vidonda.






2.Matumizi ya pombe kupita kiasi husababisha kupungua kwa uwezo wa ndani wa kuta za tumbo (Epithelial lining) kuzuia tindikali ya tumbon kutokuharibu ukuta wa ndani wa tumbo( Mucosal barrier).Hali hii hufanya tindikali pamoja na bacteria kupenya kwa urahisi kuingia kwenye kuta za tumbo na kusababisha vidonda.


stress


3. Uvutaji sigara pia waeza kupelekea kupata tatizo la vidonda vya tumbo.

4.Msongo wa mawazo



DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO

1.Maumivu ya tumbo

2. Kiungulia

3.Kupungua uzito

4.Kichefuchefu na kutapika

5.Tumbo kujaa gas

NAMNA YA KUEPUKANA NA VIDONDA VYA TUMBO

1.Epuka matumizi ya kilevi kupita kiasi


2.Epuka matumizi ya sigara

3.Tumia dawa pale unaposhauriwa na daktari.na epuka matumizi ya aspirin (NSAIDs)

4.Kula chakula bora na mlo kamili usiokuwa na tindikali nyingi.

5.Punguza msongo wa mawazo





LINKS;

1.http://www.webmd.com/digestive-disorders/tc/peptic-ulcer-disease-what-increases-your-risk

2.http://www.healthline.com/health/stomachulcer

3.http://www.mayoclinic.org/diseases-conditions/peptic-ulcer/manage/ptc-20231410

Prepared by Andrew Luhusa; MD student @ MUHAS
                            
                                     7th Oct 2016

No comments:

Post a Comment