Friday, September 30, 2016

SHINIKIZO LA DAMU (HYPERTENSION)

SHINIKIZO LA DAMU (HYPERTENSION)

Shinikizo kubwa la damu ni tatizo linalotokea katika mfumo wa mzunguko wa damu ambapo kiwango cha pressure ya damu huzidi kiwango cha kawaida ambacho huwa ni 120/80mmHg kwa mtu mzima mwenye afya nzuri.Shinikizo la damu kuwa kubwa kupita kiasi ni hatari kwa afya zetu. Tatizo huanza kuwa kubwa pale pressure ya damu inapofikia 140/90mmHg.Shinikizo kubwa la damu laweza kugawanywa katika makundi mawili kutokana na sababu za tatizo hilo, kuwa ni sababu kadhaa za kimazingira au kurithi (Esential /primary hypertension) ama kutokana na tatizo fulani kwenye mwili kwa mfano Figo kushindwa kufanya kazi (Secondary hypetension).



SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA KUPATA TATIZO LA SHINIKIZO KUBWA LA DAMU

1.Kuwa na uzito mkubwa kupita kiasi (Obesity).Uzito mkubwa kupita kiasi unatokana na kuwepo mafuta mengi mwilini kuliko yanayotakiwa mwilini.Hali hii hupelekea kurundikana kwa mafuta kwenye Organ
mbalimbali kama moyo,ini na mishipa ya damu(arteries).Hupunguza kipenyo cha mishipa ya damu na kupelekea shinikizo kubwa la damu.

2..Msongo wa mawazo (stress). kuwa  na msongo wa mawazo huathiri mfumo wa mzunguko wa damu na kufanya moyo kusukuma damu kwa nguvu, hali inayopelekea kuongezeka kwa shinikizo la damu.Hii inaweza kufanya mishipa midogo ya damu(blood carpillary) ilioko kwenye ubongo kupasuka na kupelekea kifo.




3.Matumizi ya pombe kupita kiasi. Pombe huathiri mfumo wa neva unoongoza utendaji kazi wa moyo kwa kuongeza mapigo ya moyo ( sympathetic activity ) na kupekea moyo kusukuma damu kwa nguvu na kupelekea kuongezeka kwa shinikizo la damu.


4.Matumizi ya chumvi kupita kiasi. Chumvi inapokuwa nyingi kwenye damu husababisha kusharabiwa kwa maji mengi kuingia kwenye damu na kuongeza ujazo wa damu mwilini .Hali hii hufanya kuongezeka kwa shinikizo la damu .

5.Matatizo ya figo kushindwa kufanya kazi( Renal failure). Figo inaposhindwa kufanya kazi husababisha kushindwa kuchuja damu ipasavyo.Hali hii husabisha maji mengi kubaki mwilini na kusababisha kuongezeka kwa shinikizo la damu.



DALILI ZA MTU KUWA NA SHINIKIZO KUBWA LA DAMU

Shinikizo la damu katika hatua za mwanzoni halina dalili zinazoweza kuonekana dhahiri.(asymptomatic) .Hili ni tatizo linalowapata watu wengi bila ya mtu kuona mabadiliko yoyote ambapo pressure huongezeka siku baada ya siku hatimaye kufikia katika hatua ya juu na kusababisha kifo.Katika hatua ambapo shinikizo la damu kuwa kubwa hugundulika dalili zifuatazo huambatana na mgonjwa.

  1. Maumivu ya kichwa.















    2.Kutokwa na damu puani kutokana na kuongezeka kwa pressure ya damu .









                                                                                                                                                                                                                                             
3.Maumivu ya kifua







4.Kuwa na matatizo ya macho .Hii inatokana na na kuharibiwa kwa mishipa ya damu midogo inayopeleka damu kwenye retina ya jicho inayosaidia macho kuona na hatimaye kusababisha kushindwa kuona vizuri (Hypertensive retinopathy).

5.Kuwa na uchovu na kubadilika kwa kasi ya mapigo ya moyo.


NJIA ZA KUEPUKA KUPATA SHINIKIZO KUBWA LA DAMU


  1. Fanya mazoezi ya viungo vya mwili . Njia hii hufanya mwili kuweza kuyeyusha mafuta ya ziada yaliyo kwenye mishipa ya damu na ogani nyingine mwilini ili kutoa nishati. Mazoezi pia hufanya mzunguko wa damu kuwa mzuri na kuleta afya bora.








   2. Epuka kula vyakula vyenye mafuta mengi hasa mafuta ya wanyama.(cholesterol free).Mfano kula vyakula vyenye mafuta kiasi  pamoja na kuhakikisha uwiano wa vyakula vya aina zote katika mlo kamili uko sahihi. Hii itasaidia kupunguza kuongezeka kwa kiwango cha cholesterol kwenye damu na kukuepusha kupata shinikizo la damu.



3.Epuka kunywa pombe kupita kiasi. Tabia hii itasaidia kupunguza uwezekano wa kupata shinikizo la damu kutokana na matumizi ya pombe kupitiliza .Kilevi huambatana na madhara ya muda mfupi na ya kudumu kwa afya zetu hivyo epuka pombe kupita kiasi.




4.Tumia kiasi kidogo cha chumvi kwenye chakula.

5.Punguza mambo yanayoweza kukuletea msongo wa mawazo. Hakikisha mwili wako unajishughulisha pamoja na kukaa pamoja na marafiki au vikundi vinavyojenga mawazo chanya.


LINKS

1.http://emedicine.medscape.com/article/241381-overview#a7

2.http://www.webmd.com/hypertension-high-blood-pressure/guide/hypertension-symptoms-high-blood-pressure

3.http://www.mayoclinic.org/diseases-conditions/high-blood-pressure/in-depth/high-blood-pressure/art-20046974

Prepared by Andrew Luhusa MD  Student @ MUHAS

           30th sept 2016


No comments:

Post a Comment