
SABABU ZINAZOWEZA KUPELEKEA KUPATA TATIZO LA SHINIKIZO KUBWA LA DAMU

1.Kuwa na uzito mkubwa kupita kiasi (Obesity).Uzito mkubwa kupita kiasi unatokana na kuwepo mafuta mengi mwilini kuliko yanayotakiwa mwilini.Hali hii hupelekea kurundikana kwa mafuta kwenye Organ
mbalimbali kama moyo,ini na mishipa ya damu(arteries).Hupunguza kipenyo cha mishipa ya damu na kupelekea shinikizo kubwa la damu.

3.Matumizi ya pombe kupita kiasi. Pombe huathiri mfumo wa neva unoongoza utendaji kazi wa moyo kwa kuongeza mapigo ya moyo ( sympathetic activity ) na kupekea moyo kusukuma damu kwa nguvu na kupelekea kuongezeka kwa shinikizo la damu.
4.Matumizi ya chumvi kupita kiasi. Chumvi inapokuwa nyingi kwenye damu husababisha kusharabiwa kwa maji mengi kuingia kwenye damu na kuongeza ujazo wa damu mwilini .Hali hii hufanya kuongezeka kwa shinikizo la damu .
5.Matatizo ya figo kushindwa kufanya kazi( Renal failure). Figo inaposhindwa kufanya kazi husababisha kushindwa kuchuja damu ipasavyo.Hali hii husabisha maji mengi kubaki mwilini na kusababisha kuongezeka kwa shinikizo la damu.
DALILI ZA MTU KUWA NA SHINIKIZO KUBWA LA DAMU
Shinikizo la damu katika hatua za mwanzoni halina dalili zinazoweza kuonekana dhahiri.(asymptomatic) .Hili ni tatizo linalowapata watu wengi bila ya mtu kuona mabadiliko yoyote ambapo pressure huongezeka siku baada ya siku hatimaye kufikia katika hatua ya juu na kusababisha kifo.Katika hatua ambapo shinikizo la damu kuwa kubwa hugundulika dalili zifuatazo huambatana na mgonjwa.
- Maumivu ya kichwa.

2.Kutokwa na damu puani kutokana na kuongezeka kwa pressure ya damu .
3.Maumivu ya kifua
4.Kuwa na matatizo ya macho .Hii inatokana na na kuharibiwa kwa mishipa ya damu midogo inayopeleka damu kwenye retina ya jicho inayosaidia macho kuona na hatimaye kusababisha kushindwa kuona vizuri (Hypertensive retinopathy).
5.Kuwa na uchovu na kubadilika kwa kasi ya mapigo ya moyo.
NJIA ZA KUEPUKA KUPATA SHINIKIZO KUBWA LA DAMU
- Fanya mazoezi ya viungo vya mwili . Njia hii hufanya mwili kuweza kuyeyusha mafuta ya ziada yaliyo kwenye mishipa ya damu na ogani nyingine mwilini ili kutoa nishati. Mazoezi pia hufanya mzunguko wa damu kuwa mzuri na kuleta afya bora.



4.Tumia kiasi kidogo cha chumvi kwenye chakula.
5.Punguza mambo yanayoweza kukuletea msongo wa mawazo. Hakikisha mwili wako unajishughulisha pamoja na kukaa pamoja na marafiki au vikundi vinavyojenga mawazo chanya.
LINKS
1.http://emedicine.medscape.com/article/241381-overview#a7
2.http://www.webmd.com/hypertension-high-blood-pressure/guide/hypertension-symptoms-high-blood-pressure
3.http://www.mayoclinic.org/diseases-conditions/high-blood-pressure/in-depth/high-blood-pressure/art-20046974
Prepared by Andrew Luhusa MD Student @ MUHAS
30th sept 2016