
TYPHOID
DALILI ZA MTU MWENYE TYPHOID
- Maumivu ya tumbo kwa mda mrefu
- Kushindwa kupaata choo kwa urahisi ( constipation)
- Kupanda kwa jotoridi mwili na homa (karibu 39' C au 103 F)
- Kupatwa na vidonda vidogo vyekundu(rose spots)
- kupata matatizo ya akili endapo typhoid haikutibiwa mapema
.
NJIA ZA KUENEA KWA TYPHOID
- Typhoid huenea kwa njia ya maji na chakula kama havikuandaliwa kuwa salama kwa matumizi ya binadamu. Maji machafu ni mazingira mazuri kwa ukuaji wa bacteria wa ugonjwa huu .Maji machafu kutoka chooni au mtaroni yaweza kuwa na vimelea ambavyo vimetoka kwa mtu ambaye ni mgonjwa au ambaye ametibiwa lakini vimelea vikabaki mwilini mwake (carrier). Pindi maji haya yanapochanganyika na maji safi na salama au kutumika kupika chakula ambachohakikuchemka vizuri huingia katika miili yetu.


2.Uandaaji vyakula unaweza kuwa moja ya njia ya kuenea kwa typhoid. Mtu mwenye maambukizi ya ugonjwa huu anaweza kuacha vimelea kwenye matunda na vyakula . Vyakula na matunda yaliyotayarishwa kwa njia hii huwa na uwezekano mkubwa wa kueneza typhoid.
NJIA ZA KUJIKINGA (KUZUIA) NA TYPHOID
- Osha matunda vizuri kabla ya kula.Tabia hii pamoja na kuosha viungo kama nyanya,mboga za majani na pilipili hoho kabla ya kuvipika. , itasaidia kuondoa vimelea ama kuvipunguza kabla ya kupika, hivyo kupunguza athari zinazoweza kujitokeza ikilinganishwa na kutozingatia usafi wa vitu hivi.

2. Nawa mikono kwa maji na sabuni kabla ya kula chakula,.Kunawa mikono kwa sabuni (medicated soap) kunaweza kuondoa vimelea ambavyo vingeweza kusababisha magonjwa kwa kuwa sabuni huua vijidudu vya magonjwa.


KIPINDUPINDU
![]() |
Vibrio cholerae |
DALILI ZA KIPINDUPINDU
- Kuongezeka kwa mapigo ya moyo
- Kushuka kwa shinikizo la damu
- Ngozi ya mwili kukakamaa na kupoteza uwezo wa kuvutika (elasticity)
- Kukauka mdomo na macho
- Kusikia kiu ya kunywa maji na kubanwa misuli(Muscle cramp)
Dalili hizi hutokea kutokana na kupotea kwa maji na ions kwenye mwili kutokana na kuharisha mfululizo kwa muda mrefu.
NJIA ZA KUENEA KWA KIPINDUPINDU
- Kipindupindu huenezwa hasa kupitia chakula na maji yaliyo na vimelea vya ugonjwa. Kwenye maeneo ambayo usafi hauzingatiwi ni miongoni mwa maeneo yaliyo kwenye hatari na kukumbwa na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.Mfano katika makazi ya wakimbizi ni rahisi kuchaganyika vyanzo maji safi na machafu.


3.Kula matunda pasipo kuyaosha ni hatari kwa afya zetu kwani yaweza kuwa na vimelea vya kipindupindu. Mtu atakapokula matunda huingiza na bacteria mwilini mwake ambao huweza kuleta ugonjwa huu ama magonjwa mengine kama typhoid.
NJIA ZA KUJIKINGA NA KIPINDUPINDU
- Tumia maji safi na salama
- Tumia choo kwa haja kubwa na ndogo
- Osha matunda kabla ya kula
- Epuka kula vitu maeneo yenye msongamano wa watu
LINKS:
http://www.webmd.com/a-to-z-guides/cholera-faq#1
http://emedicine.medscape.com/article/231135-medication
http://cdn.phys.org/newman/gfx/news/hires/cholerastalk.jpg
Prepared by Andrew Luhusa ;MD Student at Muhimbili University of Health and Allied Sciences(MUHAS)
15 Sept 2016
No comments:
Post a Comment