Friday, September 9, 2016

BINADAMU , MAZINGIRA NA MAGONJWA

  UHUSIANO      KATI   YA BINADAMU,              MAZINGIRA        NA      MAGONJWA

BINADAMU
Miongoni mwa viumbe hai wanaoishi duniani binadamu ni kiumbe anaechukuliwa kuwa na utashi wakuelewa mambo mbalimbali .Katika jamii yetu kila  mwanadamu amezungukwa na vitu mbalimbali ambavyo kwa ujumla wake hufanya mazingi
ra yake anayoishi.Mfano ,watu,hewa,maji na mimea hufanya maisha ya binadamu kuwa endelevu duniani.

MAZINGIRA
Jumla ya vitu vyote vinavyomzunguka mwanadamu hufanya mazingira yake yakuishi.Wanadamu tumezungukwa na na vitu mbalimbali kama vile hewa yenye gesi mbalimbali,vyanzo vya maji,ardhi pamoja na viumbe wengine wanaonekana na wasioonekana kama bacteria na virusi.


Moshi kutoka  viwandani  huchafua mazingira.






MAGONJWA
Ugonjwa ni hali ya kuwa  na afya dhaifu kutokana na kushambuliwa na vimelea vya magonjwa(pathogens) ,ukosefu wa virutubisho,sababu za urithi(genetic) na magonjwa yatokanayo na mazingira(environmental factors) .hali hii hudumaza kinga ya mwili na kupelekea hali mbaya kiafya.
       


                           ATHARI YA MAZINGIRA KWA AFYA YA BINADAMU

Hewa, maji ,chakula na mimea na vimelea kama mfano wa vitu vinavyomzgunguka mwanadamu ,vina athari kwa afya ya binadamu upale vinapochafuliwa ama kumwingia binadamu moja kwa moja(mfano,bacteria,virus na fungus).Kuchafuliwa kwa hewa kutokana na moshi wa viwanda(carbondioxide) na gesi nyingine kama sulphurdioxide huweza kusababisha magonjwa ya mfumo wa upumuaji kama vile pumu na kuongeza hatari ya kupata kifua kikuu(tuberculosis).
         Uchafuzi wa vyanzo vya maji kutokana na kemikali na kuingiliana kwa mfumo wa maji taka na maji safi ni sababu inayopeleukea magonjwa ya mlipuko  kama kipindupindu,na kuhara pamoja na typhoid. Vyakula ambavyo havikuhidhawia vizuri na ukosefu wa lishe bora ni moja ya sababu zinazopelekea baadhi ya magonjwa kama tumbo la kuharisha(dysentery),na kwashiorkor. Mazingira machafu ni makazi ya vimelea vya magonjwa kama vile bacteria na fungus .vimelelea hivi huingia ndani ya mwili na kuushambulia na hatimaye kuzorota kwa afya.
                     
                     


NJIA ZA KPUNGUZA/KUONDOA  ATHARI ZA MAZINGIRA KWA AFYA YA BINADAMU
Baada ya kuona sababu mbalimbali zinazoathiri afya ya binadamu tuangalie nini kifanyike ili kuondokana na athari zinazotokana na uhusiano kati ya mazingira yetu na afya zetu .(1)Kwanza kabisa tutambue mazingira yetu vema ili kujua namna ya kuyadhibiti,kwa mfano uwepo wa viwanda vinavyotiririsha kemikali kwenye vyanzo vya maji  karibu na maeneo yetu ya kuishi. (2)Kujenga mazoea ya kufuata kanuni za afya kutatuwezesha kuepukana na magojwa mengi , kwa mfano matumizi ya choo,kuosha matunda kabla ya kula,,kula nyama iliyoiva vizuri kuhakisha hakuna vimelea vinavyowezakuishi pamoja na kutumia maji safi na salama.(3)Kuzingatia lishe bora ni njia inayoweza kuondoa athari ambazo zingesababishwa na lishe duni kama kwashiokor kwa watoto chini ya miaka mitano,upungufu wa damu(pernicious anaemia) na magonjwa ya macho.(4)Kujifunza zaidi elimu ya afya  miili yetu ili kuongeza ufahamu juu maswala mbalimbali ya kiafya,kwa mfano kupitia mtandao kwenye blogs kama hii na semina mbalimbali za afya ya jamii.(5)Kushiriki katika  mipango mbalimbli ya afya kama vile chanjo kutakuwezesha kujikinga na magonjwa ambayo yaweza kusababisha kuzorota kwa afya yako.
              Kwa ujumla afya yako ni muhimu sana kwa ajili ya kukufanya ushiriki katika shughuli mbalimbali za kila siku.Hivyo ni tunawajibu wa kutunza afya zetu kwa ajili ya maendeleo yetu.
 Endelea kufuatialia mada ijayo uzidi kujifunza afya yako ili kukusaidia wewe na mtu mwingine.

                                               
                                     JINSI TUNAVYOPATA MAGONJWA    KUTOKA  
                                                    KWENYE MAZINGIRA YETU

REFERENCES
435,d.d24tp://scholar.google.com/scholar?q=environmental+pollution+and+tuberculosis&hl=en&as_sdt=0&as_vis=1&oi=scholart&sa=X&ved=0ahUKEwjy4I_bs4LPA

https://www.google.com/url?sa=t&rct=j&q=&esrc=s&source=web&cd=1&cad=rja&uact=8&ved=0ahUKEwil3-XXtoLPAhUBJcAKHVJbCskQFggfMAA&url=http%3A%2F%2Fwww.tanzaniatoday.co.tz%2Fnews%2Fwizara-ya-afya-yatoa-semina-kwa-wanahabari-dar&usg=AFQjCNGKIPuYA97V2VTGXnGf5HeF8jHu5A&sig2=nmU0IoGNjc_10ZoF3AYy_Q

http://www.ncbi.nlm.nih.gov/pubmed/20083235#

1 comment: